MVUA YA KIMBUNGA “CHENGE ” YATAMATIKA LEO


#breakingnews #2gendahtvonline #tma #kimbungchenge
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa ya mwenendo wa kilichokuwa Kimbunga “CHENGE” katika katika maeneo ya pwani ya nchi yetu.
Kimbunga “CHENGE” kimepoteza nguvu yake na kusambaratika kabisa wakati kikikaribia ukanda wa pwani ya nchi yetu. Hata hivyo, mvua na mawingu yaliyokuwa yakiambatana na kimbunga hicho yamesambaa katika maeneo ya ukanda wa pwani hususan katika mikoa ya Lindi, Pwani, Dar es salaam na Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba na kusababisha vipindi vya mvua katika baadhi ya maeneo hayo. Kwa mfano hadi kufika saa 12 jioni ya leo, kituo cha hali ya hewa kilichopo uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Dar es salaam kimeripoti mvua ya milimita 9.1 kwa kipindi cha saa 9 zilizopita. Vilevile katika kipindi hicho, kituo cha hali ya hewa kilichopo katika bandari ya Dar es Salaam kimeripoti mvua ya milimita 3.5.
Hashtags: #MVUA #KIMBUNGA #CHENGE #YATAMATIKA #LEO
Autor: UCE6CIkLwugZL43tLt61gtFA
Palavra Chave: meteorologia pemba
